KUWEKEZA KWA WAFANYAKAZI WAKO
Kuna
mfanyabiashara mmoja maarufu nchini marekani aliyekuwa anamiliki viwanda, reli,
meli nk jina lake ni Andrew carnegie
alisema kuwa; wakichukua mali zake zote, na biashara yake na kila
alichonacho na kumwachia wafanyakazi wake
tu baada ya miaka kadhaa atarudi kuwa na utajiri ule ule aliyo kuwa nao
mwanzo.
Unadhani
ni kwanini alisema hivyo?
Andrew
aliamini katika kuwekeza kwa wafanyakazi, aliwapa mafunzo mbali mbali na
kuwaendeleza katika taaluma tofauti tofauti. Alijenga mahusiano mazuri na
wafanyakazi wake ambayo yalipeleke kujengeka kwa imani kati yao na hivyo
kupelekea kampuni yake kukua kwa kiwango cha juu sana na yeye kuwa kati ya mabilionea nchi marekani
na duniani kote.
Je wewe
unawekeza kwa wafanyakazi wako?
Au ni
baina ya wale wanotumia ujuzi wa wafanyakazi wao bila ya kuwaendeleza na pale
wanapoona kuwa wanahitaji utaalamu mwingine zaidi ya ule waliyo nao wafanyakazi
wao wanaenda kuajiri wengine wenye
utaalamu zaidi?
Ukiwa kama mfanyabiashara naamini kuwa umekuwa ukipatwa na changamoto kubwa ya kupata wafanyakazi wazuri na kuweza kuwafanya wakae nawe kwa muda mrefu. Na kama wewe ni mfanyabishara naamini unajua umuhimu wa kuwa na mfanyakazi mmoja wakumtegemea kwenye biashara yako.
Ukiwa kama mfanyabiashara naamini kuwa umekuwa ukipatwa na changamoto kubwa ya kupata wafanyakazi wazuri na kuweza kuwafanya wakae nawe kwa muda mrefu. Na kama wewe ni mfanyabishara naamini unajua umuhimu wa kuwa na mfanyakazi mmoja wakumtegemea kwenye biashara yako.
Makampuni
makubwa nchini kutumia mbinu hii ili kuhakikisha wanatoa huduma au bidhaa nzuri
kwa wateja wao. Je si zaidi sana wewe uliye mdogo, wakati na unaye anza? Na
huwenda makampuni hayo ni washindani wako.
Tafakari
sasa na fanya mabadiliko!
- Wape nafasi wafanyakazi wako ya kujiendeleza kitaaluuma, wengi hupendelea kujiunga na masomo ya jioni katika vyuo mbali mbali . Tengeneza mazingira ya kazi ambayo hayata mbana anaye soma.
- Wapatie kozi fupi fupi ambazo unaamini zitawasaidia katika utendaji wao wa kazi. Kama cozi ya namna ya kukarimu wateja, namna ya kumhudumia mteja kwenye simu, namna ya kuelezea bidhaa au huduma unayotao kwa watu ilikumfanya mtu kuwa mateja, na mambo kadha wa kadha
- Wapatie zawadi mabali mbali kama bonas kwa wanaofanya kazi vizuri. Au pale mnapo pata ongezeko kubwa la faida.
- Kwa anaye stahili ongezeko la mshahara kwa kazi anayo fanya mpatie hata kama ni ongezeko dogo tu litampa motisha ya kuendelea kufanya kazi vizuri.
- Jenga mahusiano mazuri na wafanyakazi wako, ikibidii pata nafasi ya kuweza kuwafahamu na familia yake. Hii itakujengea ukaribu mzuri na hata kumfanya mfanyakazi wako kuona unamthamini.
- Wahusishe wafanyakazi wako katika kupanga mipango mbali mbali ya biashara yako,mawazo yao ni ya muhimu sana. Katika hili utashangaa namna mawazo yao yanavyo weza kuwa natija kubwa kwenye biashara yako.
- Usiwe na upendeleo wala kuweka madaraja kwa wafanya kazi wako, wathamini wote kwa kiwango sawa kwa kadiri uwezavyo.
Nakutakia
mwanzo mzuri wa wiki na mafanikio makubwa katika kuwekeza kwa wafanyakazi wako
na biashara yako.
Comments
Post a Comment